Friday, 4 December 2015

4. ACCOUNT IMEFUNGULIWA NMB

 YOUTH VISION GROUP

Kwa niaba ya kamati tuliyo pewa majukumu ya kusimaimia zoezi la kufungua account natanguliza SAMAHANI zoezi lime chukua muda mrefu kukamilika ni kutokana na changamoto tulizokuwa tunakutana nazo.

Habari nzuri ni kwamba tumefanikiwa kufungua account ya kikundi katika Bank ya NMB 
Kwa maelezo zaid tembelea katika email address yako.

Hivyo basi tutakuwa na kikao cha wana chama woote
siku ya Jumapili tarehe 13 december 2015. pale WHITE MARK HOTEL 

Agenda za kikao nitawatumia nikiisha kujadiliana na viongozi wenzangu


Asante.

Wednesday, 5 August 2015

3.MFANO WA VIPENGELE VYA UONGOZI NA USIMAMIZI WA CHAMA NDANI YA KATIBA


MFANO WA VIPENGELE VYA UONGOZI NA USIMAMIZI WA CHAMA NDANI YA KATIBA
TUSOME TUELEWE ILI TUTUMIE KUCHAGUA UONGOZI WA MUDA WA TAREHE 9 AUGUST 2015

1.       MKUTANO MKUU WA WANACHAMA
Kutakuwa na Mkutano Mkuu wa Wanachama wote ambao ndicho chombo cha juu cha maamuzi juu ya utendaji wa shughuli za Chama. Kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika ya Mwaka 2003 na Kanuni zake za Mwaka 2004, Mkutano Mkuu utachagua Bodi ya Chama yenye Wajumbe wasiopungua watano na wasiozidi tisa ili kuendesha na kusimamia shughuli za kila siku za Chama.

2.        BODI YA CHAMA
Kutakuwa na Bodi yenye wajumbe saba (7). Bodi itachagua Wajumbe watatu miongoni mwao kuwa Wajumbe wa Kamati ya Mikopo.

Kazi za Bodi:
a) Kusimamia shughuli za Chama kidemokrasia kwa kutilia maanani mipango na njia za kushirikiana baina ya Wanachama.
b) Kufanikisha mahitaji ya kiuchumi na kijamii ya Wanachama.
c) Kutoa elimu ya Ushirika kwa Wanachama.
d) Kuandaa miongozo sahihi ya fedha za Chama zitakazosaidia kuwepo na taarifa sahihi za mahesabu ya Chama.
e) Kuandaa Sera muhimu za Chama, kama vile Sera ya Mikopo na kuwasilisha kwenye Mkutano Mkuu kwa ajili ya kuidhinishwa.
f) Kuhakikisha hesabu za Chama zinaandaliwa na kupitiwa na Mkaguzi wa Nje kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika, Kanuni za Ushirika na Masharti ya Chama.
g) Kuwasilisha kwenye Mkutano Mkuu wa Chama hesabu zilizokaguliwa na Mkaguzi wa Nje.
h) Kuandaa makisio ya mapato na matumizi ya Chama kwa mwaka unaofuata na kuwasilisha kwenye Mkutano Mkuu kwa ajili ya kuidhinishwa.
i) Kuwezesha ukaguzi wa vitabu kwa wakaguzi wa ndani na nje kama walivyoidhinishwa na Mkutano Mkuu na kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika.
j) Kuhakikisha mikopo inaainisha dhumuni la mkopo husika.
k) Kuhakikisha Sera za Chama na Mikataba inatolewa kwa kuzingatia shughuli za Chama.
l) Kuandaa mikataba na miongozo ya kazi na masuala yahusuyo Wafanyakazi.
m) Kuajiri Meneja/Katibu na Wafanyakazi wengine wa Chama kwa mikataba endelevu ya kila baada ya miaka mitatu.
n) Kumsimamisha Mjumbe yeyote wa Bodi asiyetii matakwa ya Sheria na Masharti akisubiri maamuzi ya Mkutano Mkuu.
o) Kuhakikisha ufunguzi na kuendesha akaunti ya Chama.
p) Kutunza kitabu cha Rejista ya Wanachama.
q) Kutunza kitabu cha Rejista ya mahudhurio ya Wajumbe wa Bodi
r) Kutunza dondoo za Mikutano ya Chama.
s) Kuandaa mipango endelevu ya Chama, mpango wa biashara na kuhakikisha utekelezaji wake kwa kipindi husika.
t) Kuandaa miongozo ya uongozi wa ndani ya Chama na namna ya kutoa ripoti.
u) Kuhakikisha ina uwezo wa kujua kazi za kila siku za Meneja/Katibu na Wafanyakazi pia kusimamia akaunti ya chama.
v) Kusaini cheki za Chama.

3. MWENYEKITI WA CHAMA
Mwenyekiti wa Chama atakuwa na majukumu yafuatayo:
a) Kuwa msemaji Mkuu wa Chama.
b) Kuongoza Mikutano Mikuu ya Chama (isipokuwa Mkutano Mkuu Maalum ulioitishwa na Mrajisi na Kamati ya Usimamizi).
c) Kuongoza vikao vya Bodi.
d) Kuweka sahihi pamoja na Katibu kwenye Mikataba kwa niaba ya Chama kwa kuzingatia matakwa ya Sheria na Kanuni za Vyama vya Ushirika.
e) Kuwakilisha Chama katika Taasisi/Asasi mbalimbali ndani na nje ya Nchi.

4. MENEJA/KATIBU
Kutakuwepo Meneja ambaye ataajiriwa na Bodi na atakuwa na kazi zifuatazo:
a) Kusaidia Majukumu ya Mwenyekiti.
b) Kusimamia kazi za kila siku za Chama zinazofanywa na Wafanyakazi wengine.
c) Kuandaa malipo ya Mishahara ya Wafanyakazi na kuwasilisha kwa Bodi kwa ajili ya kuidhinishwa.
d) Kutoa taarifa za utendaji wa shughuli za Chama kwa Bodi.
e) Kuandaa au kuhakikisha inaandaliwa taarifa ya maendeleo ya Chama, hesabu za Chama za kila mwezi na taarifa nyinginezo muhimu ambazo zitasaidia Bodi kulinganisha makisio ya mwaka na matumizi yaliyotumika na pia kutoa maamuzi sahihi.
f) Kuandaa Hesabu za chama za mwisho wa mwaka na kuziwakilisha kwa Bodi pamoja na kwa Mkaguzi wa Nje.
g) Kuhakikisha vitabu vinaandikwa kwa usahihi na kuhakikisha mali za kudumu zinarekodiwa kwenye vitabu husika.
h) Kuhusika na upokeaji wa Hisa kwa Wanachama na kutoa Cheti cha Umiliki
i) Kutunza vizuri mali za Chama.
j) Kuwa Katibu wa Mikutano yote ya Chama.
k) Kutunza kitabu cha majina ya Wanachama na taarifa zao muhimu.
l) Kusaini nyaraka na mikataba ya Chama kwa niaba ya Chama.
m) Kuandaa mpango mkakati wa Chama na kuwasilisha kwa Bodi ya Chama kwa ajili ya kuidhinishwa.
n) Kusimamia utekelezaji wa mpango mkakati ulioidhinishwa na Mkutano Mkuu.
o) Kutoa mapendekezo ya marekebisho ya Masharti na Sera za Chama.
p) Kutunza taarifa za Wanachama na Wafanyakazi wa Chama.
q) Kufanya kazi nyingine zozote kama itakavyo amuliwa na Bodi.


5.       KAMATI YA USIMAMIZI
Kutakuwa na Kamati ya Usimamizi yenye wajumbe watatu (3) ambao hawatokani na Wajumbe wa Bodi ya Chama.

Kazi za Kamati ya Usimamizi:
a) Kuhakikiksha kwamba, Bodi, Kamati na Wafanyakazi wa Chama wanafuata Sheria, Masharti na Sera za Chama.
b) Kuhakikisha hesabu za Chama na vitabu vingine vya Chama ikihusisha vitabu vya Wanachama na Daftari la Wanachama vinatunzwa vizuri.
c) Kupokea na kupitia taarifa za Mkaguzi wa Ndani.
d) Kutoa ushauri kwa Bodi na Wafanyakazi wa Chama, juu ya utekelezaji bora wa shughuli za Chama na kutoa taarifa kwenye Mkutano Mkuu wa Chama.

 6.       SIFA ZA MGOMBEA
Mwanachama anayetaka kugombea uongozi katika Chama itabidi azingatie maadili ya Uongozi kwa mujibu wa kifungu Na.125 cha Sheria ya Vyama vya Ushirika Na.20 ya Mwaka 2003.

Sifa za kugombea:
a) Awe na upeo na elimu ya kutosha kuweza kuongoza Chama kulingana na mabadiliko ya hali ya uchumi wa nchi.
b) Awe ni mfuatiliaji wa shughuli za Chama kwa kutekeleza wajibu wake katika Chama na kwa kuzingatia Sheria ya Vyama vya Ushirika, Kanuni na Masharti ya Chama.
c) Awe ni mtu mwenye ari ya kutoa mchango wake wenye nia ya kuendeleza Chama endapo atachaguliwa kuwa Kiongozi.
d) Awe na ufahamu wa shughuli za Ushirika.
e) Awe mwaminifu na si mpenda kupokea wala kutoa rushwa.
f) Awe ni mtu ambaye hajawahi kuenguliwa katika uongozi katika Chama chochote cha Ushirika kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu.
g) Awe Mwanachama hai kwa kulipa kiingilio na Hisa zote zinazotakiwa kwa mujibu wa Masharti ya Chama.
h) Awe anashiriki kikamilifu katika shughuli za Chama.
i) Awe ni Mwanachama katika kipindi kisichopungua mwaka mmoja.
j) Awe ameajiriwa na sekta rasmi na pia awe anapatikana kwa urahisi.

Tuesday, 28 July 2015

2.PICHA MBALIMBALI ZA WANACHAMA WAKATI WA KIKAO TAREHE 26 JULY 2015


                                         JULIUS NA HABIL WAKITETA JAMBO

                                        
 ABDULY NA GEORGINA KATIKA POZI

 
BARAKA KUNA KICHWA MAMBO MAGUMU

 
WATU KAZINI

 
 
KAZI INAENDELEA

 
SEHEMU TULIPO KUTANA

 
TIGO NAO WALIKUWEPO

 
WAKATI WA KUPITIA RATIBA


1. SACCOS NI NINI?


SACCOS  NI NINI?


 NENO SACCOS Ni Ufupisho wa maneno ya Kiingereza yafuatayo:

Savings (SA)

Credit (C)

Co-operative (Co)

Society (s)

 Maneno haya ndiyo huunda neno moja  SACCOS  yaani Savings and Credit Cooperative Society.  Kwa  kiswahili  tafsiri rasmi ni chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo.

 CHAMA CHA USHIRIKA NI NINI?

 Kwa mujibu wa  tafsiri  iliyotolewa na Wizara ya Ushirika na Masoko Februari 2003 katika sera ya maendeleo ya ushirika.

Chama cha ushirika ni Muungano wa watu waliojiunga pamoja, kwa hiari kwa madhumuni ya kufanikisha mahitaji yao kwa kuanzisha na kumiliki chombo chao kidemokrasia na kuchangia mtaji unaohitajika kwa usawa na kukubali kuyakabili  matatizo na kupata manufaa kutokana na shughuli zake ambazo  wao hushiriki kikamilifu.

 SIFA  ZA  KIPEKEE ZA CHAMA CHA USHIRIKA ZIPO SIFA KUU 4 ZINAZOUPA USHIRIKA SIFA ZA  UPEKEE:

1.  Ni  Taasisi inayoongozwa na kundi la watu  (Controlled by an association of persons)

2.  Ni Taasisi inayoweza  miongoni mwa wanachama wake  kuwa na watumiaji wa aina moja au zaidi wa  huduma zake (watoaji na wapokea huduma)

3.  Lengo kuu la ushirika siyo kupata faida kubwa  au kuibadili jamii ila kukuza maslahi ya wanachama wanayoyapata kwa kufanya biashara na chama chao cha ushirika.

4.  Huongozwa na Masharti mtaalum yanayohakikisha  usawa katika kugawana madaraka (equality in distribution of power) na  uwiano  sawa  katika kugawana  mali ya chama (equity in distribution of assets).  Haya hutekelezwa kwa kuzingatia misingi  5 ya ushirika.

v  Uwajibikaji

v Demokrasia

v Usawa

v Kuchangia kwa usawa

v Mshikamano

 
KANUNI MPYA ZA USHIRIKA

1.Uanachama  wa wazi na hiari

2.    Udhibiti wa kidemokrasia wa wanachama

3.    Ushiriki wa  kiuchumi wa wanachama.

4.    Uhuru na kujitegemea

5.    Elimu, mafunzo na habari

6.    Ushirikiano baina ya wanaushirika

7.    Kujali jamii

 

SACCOS  nini basi?

Ni :


§  Asasi ya kifedha inayomilikiwa na kuongozwa na muungano wa watu.

§  Asasi inayomilikiwa kwa pamoja kati ya waweka Akiba na Wakopaji.

§  Ni asasi  ya kifedha yenye malengo tofauti na yale ya kibenki yanayolenga kukuza faida za ushirika kwa wanachama wake kupitia akiba zao na mikopo yao,

§  Asasi inayoendeshwa kwa kutumia kanuni maalum

 
BODI ANZILISHI INATAKIWA KUFANYA NINI?

Bodi anzishlishi ya SACCOS huchaguliwa katika Mkutano anzilishi unaongozwa na Afisa Ushirika (W) au Afisa Ushirika yoytoe aliyeteuliwa na  Mrajiri wa vyama vya Ushirika nchini.

 Kamati itakuwa na wajumbe 5 hadi 9. Kamati anzilishi itachagua kutoka  miongoni mwao Mwenyekiti na kumteua Katibu na  kutunza kumbu kumbu zake.

 KAZI ZA BODI ANZILISHI

(a)         Kuangalia/Kuamua aina ya chama wanachama  wanachotaka  kukianzisha kwa kina na madhumuni/malengo yake.

(b)        Kutathmini; Ukubwa wa biashara ya wanachama waanzilishi.

(c)         Kufanya  tathmini ya wanachama watarajiwa na kiwango cha biashara  tarajiwa.

(d)        Kufanya upembuzi yakinifu wa kiuchumi na shughuli za kiutendaji zinazotarajiwa kufanywa na chama husika kwa kushirikiana na Afisa Ushirika au mtu mwingine yeyote mwenye ujuzi husika.

(e)         Kuandaa orodha ya wananchama waanzilishi na kumbukumbu za hisa/mtaji wa chama na michango kama ilivyopendekezwa katika masharti ya chama.

(f)          Kuandaa orodha ya wanachama watarajiwa na kumbukumbu za mtaji au michango yao.

(g)         Kuandaa  masharti ya chama chao kwa kushirikiana na Afisa ushirika.

(h)        Kufanya jambo lolote  muhimu ili kuwezesha/kufanikisha uandikishaji wa chama tarajiwa.

 SOTE TUNAJUA FAIDA ZA USHIRIKA WA  KUWEKA NA KUKOPA. TUUNGANE TUANZISHE SACCOS YETU.